Pages

ALICHOKISEMA NAPE NNAUYE KUHUSU KAULI ILIYOTOLEWA NA EZEKIEL MAIGE

Jun 1, 2012
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Nape Nnauye amezungumzia taarifa zilizo andikwa na baadhi ya Magazeti ya jana kuhusu kilichosemwa na aliyewahi kuwa waziri wa Nape amesema shutuma alizozitoa Maige, kwanza ikumbukwe kwanza yeye ni Mbunge anaewakilisha Jimbo, juu ya jimbo kuna wilaya na mkoa lakini kama mwanachama ana tawi,Kata na kuna shina ambalo anatoka sasa ukiangalia kwenye level alipo yeye na level nilipo mimi mjumbe wa kamati kuu na katibu mwenyezi wa Taifa wa chama nikianza na mimi kumjibu hadharani nitakua simtendei haki kwa sababu kwakweli sio saizi yangu, naacha vikao vinavyohusika huko chini vishughulike nae na wakifikia mahali wameshindwa basi watatuletea tutashughulika naeMaliasili na Utalii Ezekiel Nnauye amesema kuhusu hili swala la kusema wanachama karibu elfu ngapi wameondoka, ni kwamba CCM ina wanachama wengi sana na hawajaanza leo kuondoka kutoka CCM, hakuna chama hata kimoja cha Siasa nchini ambacho kimeanzishwa na wanachama ambao hawakutoka CCM, ukianza mwaka 1992 tulipoanzisha mfumo wa vyama vingi wanachama wote walioanzisha vyama vingi walitoka CCM kwa hiyo ni jambo ambalo limefanyika kwa miaka 20 na CCM haijafa, kwa hiyo leo kuwadanganya wanaccm na Watanzania kwamba eti kwa sababu kuna watu wawili watatu wamehama kutoka CCM kwenda vyama vingine CCM inakufa, huu ni uongo wa mchana kweupe


Maige.