Pages

MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA SERIKALI ZA MITAA 2012

Jun 26, 2012


Sherehe za maadhimisho ya siku ya Serikali za mitaa zinafanyika jijini Mwanza, sherehe zikifanyika kwa ushirikiano wa jumuiya za serikali za mitaa Alat na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI.
 Maadhimisho hayo yanafanyika sasa katika uwanja wa CCM Kirumba tangu tarehe 24 juni hadi tarehe 1 july 2012 na kuhusisha shughuli mbalimbali mathalani Kongamano la kuboresha ubia baina ya sekta za Umma na Binafsi. 

 Wananchi wakiwa katika banda mojawapo uwanjani humo wakionja ladha ya mvinyo mmoja wapo unaotengenezwa na viwanda vidogo hapa nchini.

 Kauli mbiu kwa maadhimisho haya kwa mwaka huu ni 'Shiriki sensa ya watu toa maoni kuhusu katiba mpya kuharakisha ugatuaji wa madaraka kwa wananchi kwa maendeleo yao'

 Ufugaji bora nao unahusishwa kwenye maonyesho haya.

Wananchi kwenye baadhi ya mabanda.

Ramani picha ikionesha mpango wa jinsi jiji la Mwanza litakavyokuwa kufikia mwaka 2025.