Pages

HUYU NDIYE MUHUBIRI MAARUFU DUNIANI KWA KUTABIRI AJALI

Jul 18, 2012

Muhubiri TB Joshua wa Nigeria ametabiri tena kwamba kuna ajali nyingine mbaya ya ndege itakayotokea siku za karibuni kwenye nchi hiyo.
Amesema kama hiyo ajali ya ndege haitotokea basi wanasiasa tisa  mpaka 12 wa Nigeria watapoteza maisha yao kwenye ajali nyingine ya ndege, na hiyo itatokea wakati wakiwa wanarudi kutoka kwenye mkutano.
Yani wote watapoteza maisha kwenye ndege itakayokua imewabeba wakiwa kuanzia 9 mpaka 12 kwa sababu shetani ana mipango ya kuwashambulia wote kwenye ndege hiyo moja.
Amesema ili kuepuka hiyo ajali ni lazima wanasiasa hao waepuke kupanda ndege moja.
Mtandao wa Naija umeuliza, kama kweli huyu ni mtumishi wa Mungu na anaweza kutabiri mambo mabaya tu kutokea kwenye nchi hiyo, kwa nini asitumie nguvu yake kuomba neema na Nigeria kuepushwa na hayo majanga?
Hii ndio ajali maba ya ndege iliyotokea June 4 mwaka huu na kuua zaidi ya watu 153.