Pages

MATUKIO YA UOKOAJI KATIKA AJALI YA MELI ULIVYOKUA

Jul 18, 2012

 Waokoaji wakiwa kazini kwenye Meli ya Kilimanjaro



                                       Muokoaji akiwa na maiti
 
Majeruhi wa wakipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Mnazi Mmoja
MV KMKM ikiwa kazini


Raia wa kigeni wakiwasili Bandarini baada ya kuokolewa


Majeruhi wakipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mnazi Mmoja


Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imesema, meli iliyozama jana katika kisiwa cha Chumbe, Zanzibar ilikuwa na abiria 248 wakiwemo watoto 31. 

Kwa mujibu wa Sumatra, meli hiyo, inamilikiwa na Kampuni Seagul Transport, imasajiliwa na Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA) na kwamba, Cheti cha Ubora kimeanza tarehe 24 Agosti, 2011 na kinamalizika 23 Agosti, 2012. Imesema, meli hiyo ilikuwa imeruhusiwa kubeba abiria wanaoruhusiwa 300 na tani 26 za mizigo.

SUMATRA kupitia Kituo cha Utafutaji na Uokoaji (MRCC) ilipata taarifa kuwa meli ya MV Skagit iliyokuwa safarini kutoka Dar es Salaam kuelekea Zanzibar ilikuwa inazama katika eneo la karibu na kisiwa cha Chumbe, Zanzibar, eneo ambalo lipo umbali wa Kilomita za Bahari 13.8 kutoka Bandari ya Zanzibar.

Zoezi la uokoaji linaendelea katika eneo la tukio kutoka kwa Mv Flying Horse, Mv Kilimanjaro III, Tug Bandari ya Zanzibar, KMKM, Mv Zanzibar I, Police Patrol Boat, Navy.

Chanzo:www.francisgodwin.blogspot.com