Pages

HAMISI KIZA KUONDOKA YANGA LEO

Nov 16, 2012

Mshambuliaji wa Yanga, Hamisi Friday Kiiza 'Diego' (pchani), anatarajiwa kuondoka leo saa 11:00 jioni mjini Dar es Salaam kwenda Kampala, Uganda kujiunga na timu yake ya taifa, The Cranes kwa ajili ya kambi ya kujiandaa na michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, Tusker Challenge itakayofanyika mwishoni mwa mwezi huu hadi mwanzoni mwa mwezi ujao mjini Kampala. Kiiza aliyewezesha Yanga kuongoza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacoim Tanzania Bara, anaondoka akiwa katika kiwango kizuri kwenda kuisaidia Uganda kutetea taji lake ililotwaa mwaka jana Dar es Salaam wakiifunga Rwanda katika fainali.