Pages

ISIKILIZE RIPOTI NYINGINE YA MWANDISHI AKIWA TEMEKE HOSP AMBAKO INAAMINIKA KUNA WATU WAMEGANDANA WAKIFANYA MAPENZI, POLISI WAMEANZA KUTUMIA MABOMU.

Nov 8, 2012

Hii ndio ripoti ya mwandishi Salehe Masoud wa Clouds tv kuhusu taarifa ya miili ya watu kung’ang’ania wakiwa gest house baada ya kufumaniwa, yani ni mwanaume aliekutwa na mke wa mtu ambapo Masoud ambae yuko kwenye hospitali ya Temeke ambako watu hao wanadaiwa kupelekwa ameripoti kwamba baadhi ya mashuhuda wanasema watu hao wamefikishwa hospitali wakiwa wamegandana na waliteremshwa kwenye gari wakiwa hivyohivyo ingawa uongozi wa hospitali umekanusha na tayari umeshatoa tamko kwa mamia ya watu waliokusanyika kwamba sio la kweli, hakuna ukweli wa hizo taarifa.
Baada ya watu kuzidi kuwa wengi na kila mmoja akitaka kuona hao waliogandana, polisi wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kutawanya mamia ya watu waliofika kushuhudia ambapo inasemekana wawili hao wamehifadhiwa nyuma ya Mochwari.
Hao watu inasemekana walikutwa wakifanya mapenzi kwenye nyumba moja ya wageni huko Temeke 
CHANZO NI MILLARD AYO.COM