Pages

BAADA YA MTAJI, SASA DOGO ASLAY ANAMJENGEA MAMA NYUMBA

May 31, 2012
Dogo Asley November mwaka jana alimpa mama yake mtaji wa laki tano kwa ajili ya kufanya biashara, leo ametangaza good news nyingine kuhusu kuwasaidia wazazi wake ambao maisha yao yamebadilika kwa kiasi kikubwa baada ya kupewa mitaji ambayo wameweza kuiendeleza vizuri mpaka sasa.
Alichokitangaza leo Dogo Aslay mwenye umri wa miaka 16 ambae muziki pekee ndio unaompa hela, ni kuhusu kuwasaidia wazazi wake kujenga nyumba kwenye kiwanja ambacho kilinunuliwa na mama yake mzazi Gongo la Mboto Dar es salaam miaka kadhaa iliyopita, ametoa zaidi ya laki saba Mwaka huu kuifikisha nyumba mpaka kwenye madirisha na anachotaka ni kumaliza kuijenga ndani ya muda mfupi sana ujaoHiki sio kitu cha kawaida, dogo Asley amekua mtoto wa kwanza Tanzania mimi kumsikia akiwa na umri mdogo kama huo lakini katoa kiwango kiwango kikubwa cha pesa kama hicho kumjengea mama yake nyumba.
skiliza track yake mpya hapo chini