Pages

HAWA NDIO WASHIRIKI WAWILI WA BIG BROTHER WALIOTOKA GHAFLA KWENYE JUMBA

May 18, 2012


Mashabiki wa shindano la Big Brother Afrika, leo tena wamepata pigo jingine baada ya Washiriki wa Nigeria, Ola na Chris kuomba kujitoa kwenye shindano hilo ambapo hiyo imetokana na Ola ambae anadaiwa kuwa mgonjwa wa bp kuwa dawa alizopewa hazijafanya kazi hivyo ni lazima atoke kwenye jumba la big brother ili kuwa karibu zaidi na matibabu ya uhakika Chris ambae ni mshiriki mwenzake walietoka pamoja kwenye jumba hilo, amehuzunika sana kwa kilichotokea kwa mwenzake na kukiri kwamba anaelewa, walikua kwenye mashindano wakicheza pamoja lakini hawawezi kucheza na maisha yao Baada ya ombi hilo Big Bro aliwakubalia kuondoka, na ikabidi wawaage washiriki wenzao leo leo na kuondoka japo wenzao waliwaruhuru kuondoka kutokana na hali halisi, huzuni ilitawala, washiriki wengine waliobaki walihuzunika sana na wengine hata kulia kabisa kwa sababu bado walipenda kuendelea kukaa na Chris na Washiriki hao wawili wanakamilisha idadi ya washiriki watano walioondoka ndani ya jumba hilo kwa mwaka huu wakiwemoa watanzania wawili pamoja na mzimbabwe mmoja japo Chris na Ola wametoka bila utaratibu wa kawaida wa washiriki kutolewa kwenye jumba hilo ambapo huwa ni kila jumapili